Thursday, October 25, 2012

NAPENDA KUTOA NAFASI HII KUTOA SHUKRANI ZANGU ZA DHATI KWA....

WADHAMINI wangu wa nguvu Tsn supermarket kiukweli wamenipa sapoti ya kweli mpaka nashindwa nisemeje.Kina dada au mama endelea kutembelea matawi yao yaliyopo mikocheni baraka plaza,upanga,bamaga na tegeta kwa mahitaji mbalimbali. Clouds fm radio team nzima ya power breakfast ikiongozwa na Gerald Hando,Seba Maganga(pm),Sheba Kusaga,Rose Nyanje,Joyce Shebe,Asma Makau na Gea Habib.
Nawashukuru sana Bloggers wenzangu blog zifuatazo
www.8020fashions.blogspot.com
www.kajunason.blogspot.com
www.michuzijr.blogspot.com
www.misspopuler.blogspot.com
www.adeladallykavishe.com
www.homezdeco.blogspot.com
www.modewji.blospot.com
www.mjengwa.blogspot.com
duhhhhh ni nyingi sana mpaka nyingine nimezisahau.Nawashukuru sana I view media kwa my bro Raque kwa kazi ya atwork kwa ujumla,Mawesu printers walioprint billboards zangu.Shekinah garden walitupa nafasi ya kujumuika nao katika pre event dinner kule mbezi Makonde.
Skylite Band kutoka kwa my bro Sebastian Ndege,Zamda Geogre kwa kutubunia nguo nzuri toka tunaanza kupiga picha za theme mpaka wadada walikuwa wakitoa huduma siku ya event.Marafiki zangu wote ambao nilikuwa nikiwasumbua kwa hili na lile nawashukuru sana Janet Matola mweee sijui ningewezaje bila wewe, na Asma Makau.
Katika shughuli yoyote hakukosekani mapungufu tuliyaona na tunatarekebisha kwa ajili ya wakati ujao.

MATARAJIO
Mwakani mambo mengi yatabadilika sana kulingana na maoni na mahitaji yako mdau wa kitchen party gala.Mikoani pia tutafika tunaanza na Arusha tarehe 10 mwezi ujao itakuwa jumamosi pale tripple A kwa kiingilio kile kile cha 30,000.Mwezi december tutakuja Mwanza.Kama unataka kudhamini kwa namna yoyote ile unakaribishwa.
Kwa niaba ya my patner Vida Mndolwa ambae kipindi hiki hakuonekana alikuwa ameenda kujifungua mtamuona mwakani.Tunasema Asante sana kwa wote kwa kufanikisha hasa wewe uliyekuja.

No comments:

Post a Comment