Tuesday, December 4, 2012

NAMSHUKURU MUNGU KILA SIKU NATENGENEZA FAMILIA NA MARAFIKI WAPYA.

 Jana nilipata mgeni kutoka Mbeya amekuja Dar es salaam kwa shughuli zake.Lakini moja ya malengo yake ni kuja mpaka clouds fm kukutana na mimi.
 Anaitwa Lucy Komba,nikampokea na kumtembeza mjengoni kwetu na akakutana na watangazaji mbali mbali kama alivyoonekana kwenye picha ya kwanza akiwa na Millard Ayo.Jana ilikuwa blue monday basi nimekurupuka kuja ofisini maana jana yake tulikuwa kwenye party ya miaka 13 ya clouds fm kulala asubuhi na hapo hapo uamke kwenda ofisini wanaleo tena wanakusubiri nilikomaje.
 Mgeni wangu hakuwa mikono mitupu,akanipa zawadi ya kanga hii nzuri.Namshukuru Mungu kwa hilo kwani naongeza marafiki nafamilia kila siku.
Ni kweli kabisa Wema wa Mungu upo kila siku.

No comments:

Post a Comment