Thursday, November 29, 2012

UZINDUZI WA TUSKER LITE NDANI YA USIKU WA MAAFISA MASOKO

 Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni ya bia ya Serengeti (SBL), Steve Gannon akinyanyua juu bia mpya ya Tusker Lite wakati wa uzinduzi wake rasmi uliofanyika mbele ya maafisa masoko wa makampuni mbalimbali nchini wakati wa tafrija maalum ya ‘Markerts Night’ jijini Dar es Salaam jana. 

Mkurugenzi Masoko wa Kampuni ya bia ya Serengeti (SBL), Epraim Mafuru akizungmza mara baada ya uzinduzi wa bia mpya ya Tusker Lite wakati wa uzinduzi wake rasmi uliofanyika mbele ya maafisa masoko wa makampuni mbalimbali nchini wakati wa tafrija maalum ya ‘Markerts Night’ jijini Dar es Salaam jana.

Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni ya bia ya Serengeti,Steve Gannon (wapili kulia) , akiwa pamoja na wafanyakazi wa SBL wakigonganisha chupa zao za Tusker Lite kuashiria furaha ya kuzinduliwa kwa  bia hiyo mpy. Tusker Lite ilizinduliwa wakati wa tafrija maalum ya ‘Markerts Night’ jijini Dar es Salaam jana.




Baadhi ya wafanyakazi wa Kampuni ya bia ya Serengeti (SBL) wakifuatilia matukio mbalimbali wakati bia mpya ya Tusker Lite ilipozinduliwa sanjari na usiku maalum wa maafisa masoko jijini Dar es Salaam jana. 


Mkurugenzi wa Masoko wa Kampuni ya Bia ya Serengeti (SBL), Epraim Mafuru (mwenye suti kushoto) akimkabidhi zawadi ya Tusker Lite, Meneja bidhaa wa Push Mobile, Gonzoga Rugambwa  baada ya kuibuka mshindi wa kwanza wa shindano maalum la uchezaji mziki lililofabnyika wakati wa uzinduzi wa bia ya Tusker Lite sanjari na usiku wa maafisa masoko jijini Dar es Salaam jana.

Wafanyakazi wa kampuni ya Bia ya Serengeti (SBL) wakiwa na mmoja wa washindi wa shindano maalum la uchezaji mziki lililofanyika katika usiku maalum wa Maafisa masoko jijini Dar es Salaam jana. Mshindi huyo wa pili alizawadiwa Glass maalum ya Tusker Lite, bia mpya iliyozinduliwa usiku huo.
 
Vijana wa sarakasi wakionesha ufundi wao wakati wa tafrija ya maalum ya Maafisa masoko na uzinduzi wa bia mpya ya Tusker Lite inayozalisha na kusambazwa na Kampuni ya Bia ya Serengeti. (Picha na Mpigapicha wetu).

No comments:

Post a Comment